Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kupitia Afisa Habari wake, Clifford Mario Ndimbo, limetangaza viingilio vya mechi ya marudiano ya Kufuzu AFCON2025 kati ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya DR Congo.
Ndimbo amesema kuwa katika majukwaa ya mzunguko kiingilio ni shilingi 2,000 na katika jukwa la VIP ‘B’ na ‘C’ itakuwa Tsh ni 5,000 tu.
Akizungumza katika hamasa ya kuelekea mchezo huo, Ndimbo amesema kuwa kwa sasa akili inapaswa kuelekezwa kwenye mchezo huo utakaopigwa Jumanne ya October 15, 2024 na kusahau matokeo ya ya mchezo wa Kwanza ambao Tanzania imefungwa bao 1-0.