SIFA za Kujiunga na Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI)

SIFA za Kujiunga na Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI)
SIFA za Kujiunga na Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI)

Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo kilichopo Dodoma ni taasisi ya elimu inayotoa mafunzo mbalimbali kwa lengo la kuimarisha ujuzi na maarifa katika usimamizi wa serikali za mitaa na maendeleo ya jamii.

Chuo hiki kinatoa kozi mbalimbali zinazolenga kuboresha utendaji kazi wa watumishi wa umma na sekta binafsi.

Namna ya Kuomba Kujiunga na Masomo Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI)
  • Astashahada (NTA Level 4 - Basic Technician Certificate)
Sifa za Kujiunga na Masomo Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI) 

Sifa za kujiunga na kozi mbalimbali katika Chuo cha Serikali za Mitaa Hombolo zinatofautiana kulingana na ngazi ya kozi.

Ngazi ya Cheti (NTA Level 4)
Sifa za Kujiunga:
  • Kidato cha Nne (Form Four) na ufaulu wa angalau daraja la nne (Division IV).

Ngazi ya Diploma (NTA Level 5)
Sifa za Kujiunga:
  • Mwombaji awe amepata angalau ufaulu wa “Principal Pass” moja na “Subsidiary” katika mtihani wa Kidato cha Sita (ACSEE) AU awe na Astashahada (NTA Level 4 Basic Technician Certificate) toka Chuo chochote kilichosajiliwa na kinachombulika na Serikali. 
  • Pia awe amepata angalau ufaulu wa “D” 4 za Kidato cha Nne(CSEE). Masomo ya Dini hayahusiki.
Ngazi ya Diploma ya Juu (NTA Level 6)
Sifa za Kujiunga:
  • Kidato cha Nne (Form Four) na ufaulu wa angalau daraja la nne (Division IV) na diploma ya NTA Level 5 katika kozi husika.
ANGALIZO:
  • Kozi ya Uhasibu na Fedha katika Serikali za Mitaa (Local Government Accounting and Finance) inahitaji mwombaji awe amefaulu somo la HISABATI katika mtihani wake wa kidato cha nne.
  • Kama mwombaji amefanya mtihani wa kidato cha nne zaidi ya mara moja, aambatanishe nakala za vyeti vyake vya awamu zote za mithani aliyofanya.
Gharama za masomo na mchanganuo wa ada unapatikana katika ukurasa wa 
tatu(3) wa fomu ya maombi.

Fomu zinapatikana:
  • Chuoni, Hombolo
  • Kampasi ya Dodoma Mjini (Area C)
  • Katika tovuti ya Chuo www.lgti.ac.tz
  • Wizarani Ofisi ya Rais-TAMISEMI (Library)
Fomu iliyokwisha jazwa iambatanishwe na malipo ya ada ya maombi ya shilingi 
10,000/=kwenye Akaunti Na. 50501100209 NMB. Jina la akaunti ni CHUO CHA 
SERIKALI ZA MITAA

Taarifa zaidi Tembelea Website ya Chuo cha Serikali za Mitaa http://www.lgti.ac.tz
Post a Comment (0)
Previous Post Next Post

PATA NYIMBO ZOTE MPYA BONYEZA HAPA

 

MATANGAZO YA BIASHARA WASILIANA NASI KUPITIA nijuzehabariblog@gmail.com

 

JIUNGE NA GROUP ZETU HAPA CHINI UPATE FURSA KAMA HIZI KILA SIKU.

 

GROUP LA WHATSAPP NO 1 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 2 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 3 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 4 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 5 BOFYA HAPA