Nifanye nini ninaposhuhudia uhalifu?
- Piga namba ya dharura bure 111 or 112 haraka na utoe maelezo kwa ufupi juu ya tukio hilo.
Haki zangu ni zipi ninapo simamishwa na Askari Polisi?
- Una haki ya kuwatambua askari kwa vitambulisho, kujua kosa au sababu ya kusimamishwa.
Nawezaje kuripoti jambo linalotia mashaka?
- Wasiliana na Akari au kituo cha Polisi karibu nawe au piga simu bure 112 au 112.
Naweza kuripoti tukio la kihalifu mtandaoni?
- Ndio kwa kujaza fomu maalum ya kuripoti matukio
- RIPOTI TUKIO
Nifanye nini ikiwa mimi ni mhanga wa Uhalifu?
- Wasiliana na Polisi na utafute msaada wa matibabu kama kuna ulazima
- Contact the police and seek medical attention if necessary.
Nawezaje kupata ripoti ya kupoteza mali
- Utajaza taarifa zako kwenye mfumo kwa vitu vya kielekroniki kama simu nk, vitambulisho utaweza kupakua na kuprint popote ulipo.
- Kwa vitu vya thamani kubwa utalazimika kufika kwenye kituo kilicho karibu yako kwa msaada zaidi.
Nawezaje kutoa taarifa za unyanyasaji wa kijinsia
- Wasiliana na Dawati la jinsia jeshi la polisi katika ktuo kilicho karibu nawe au piga namba zifuatazo +255 787 668 306