Katika orodha hii mpya Klabu ya Simba ya Tanzania imeshuka hadi nafasi ya 7 kutoka nafasi ya 5 ikiwa na pointi 39 sawa na Petro de Luanda ya Angola zikiwa zimezidiwa na timu za Al Ahly ya Misri ambao ni Mabingwa wenye pointi 87.
Timu zingine zilizo juu ya Simba ni Espérance de Tunis ya Tunia wenye pointi 61, Wydad Casablanca ya Morocco pointi 60, Mamelodi Sundowns ya South Africa pointi 54, Zamalek SC ya Misri ambao ni Mabingwa wa Kombe la Shirikisho yenye Pointi 48 na RS Berkane ya Morocco yenye pointi 42.
VILABU 30 BORA AFRIKA 2023/2024 (CAF CLUB RANKING)
Klabu nyingine ya Tanzania Young Africans wao kwenye Club ranking wameshuka hadi nafasi ya 13 kutoka nafasi ya 12 wakiwa na pointi 31.
Orodha Kamili ya Vilabu 30 Bora msimu wa 2023/24 Kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) ni kama ifuatavyo;
- Al Ahly SC - Egypt = 87.
- Espérance de Tunis - Tunisia = 61
- Wydad Athletic - Morocco = 60.
- Mamelodi - South Africa = 54.
- Zamalek SC - Egypt = 48.
- RS Berkane - Morocco = 42.
- Simba SC - Tanzania = 39.
- Petro de Atletico - Angola = 39.
- TP Mazembe - DR Congo = 38.
- CR Belouizdad - Algeria = 37.
- USM Alger - Algeria = 36.
- Raja Casablanca - Morocco = 35.
- Young Africans - Tanzania = 31.
- ASEC Mimosas - Ivory Coast = 30.
- Pyramids FC - Egypt = 29.
- Al Hilal Omdurman - Sudan = 25.
- JS Kabyilie = Algerian = 22.
- Rivers United - Nigeria = 18.
- Horoya Athletic - Guinea = 18
- Etoile du Sahel - Tunisia = 16.
- Orlando Pirates - South Africa = 16
- Dreams FC - Ghana = 15.
- ES Sétif - Algeria - 14.
- Modern Future FC - Egypt = 12.
- Marumo Giallants - South Africa = 12
- Coton Sport FC - Cameroon = 11.5.
- FC Nouadhibou - Mauritania = 10.5.
- Abu Salem SC - Libya = 10.
- Stade Malien - Mali = 10
- Kaizer Chiefs - South Africa = 10.