VIINGILIO YANGA VS CBE SA 21 SEPTEMBER 2024
Viingilio vya mchezo wa pili kuwania kufuzu hatua ya Makundi ya CAF Champions League 2024/2025 kati ya Young Africans dhidi ya CBE SA ya Ethiopia.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumamosi hii ya tarehe 21 September 2024 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzibar Kuanzia Saa 2:30 Usiku.
Kuelekea mchezo huo, hivi hapa chini ni viingilio ambavyo vitakuwezesha kuingia uwanjani kuishabikia klabu yako wakati ikisaka nafasi ya kutinga Makundi ya Klabu Bingwa Afrika 2024/2025.
Uongozi wa Young Africans umekitaja kiingilio cha Tsh 5,000 tu kuwa ndicho kiingilio cha chini zaidi kwenye mchezo huo.
Viingilio vingine vitakuwa Tsh 10,000 (ORBIT), Tsh 15,000 (URUSI), Tsh 20,000 (WINGS) na Tsh 30,000 Kwa VIP A.