Kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 27 November 2024 hizi hapa ni Sifa za Mpiga Kura.
- Awe raia wa Tanzania.
- Awe na umri wa miaka 18 au zaidi.
- Awe ni mkazi wa eneo la kitongoji.
- Asiwe na ugonjwa wa akili uliothibitishwa na Daktari anayetambulika na Serikali au bodi ya utabibu.
- Awe amejiandikisha kupiga Kura katika kitongoji husika na
- Awe na akili timamu.