Tafadhali rejea kichwa cha habari pamoja na barua yangu yenye Kumb Na. AB. 161/259/01/A/41 ya tarehe 06 Juni, 2022 kuhusu somo tajwa hapo juu.
Napenda kukutaarifu kwamba, Sekretarieti ya Ajira imeandaa ratiba ya usaili wa kada zilizokasimiwa unatarajia kufanyika kuanzia tarehe 26 Septemba - 02 Oktoba, 2024.
Kila Mwajiri anapaswa kuzingatia ratiba hiyo, ikiwa ni pamoja na kufanya maandalizi ya usaili mapema ikiwemo kutoa tangazo la kuitwa kwenye usaili waombaji kazi wote waliopendekezwa kulingana na kada zilizotangazwa likiwa limeainisha aina ya vitambulisho anavyopaswa kuja navyo msailiwa kwaajili ya utambuzi wakati wa usaili (Vitambulisho hivyo ni pamoja na Kitambulisho cha Taifa (NIDA), Kitambulisho cha Mpiga kura, Kitambulisho cha Mkazi, Hati ya kusafiria, Leseni ya Udereva na barua ya utambulisho toka Serikali ya Kijiji/Mtaa.
Pamoja na barua hii naambatisha ratiba na orodha ya Halmashauri thelathini na moja (31) zitakazoendesha usaili huo.