Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limetangaza kuwa mechi za Ngao ya Jamii kwa upande wa Wanawake zitapigwa October 02-05, 2024 Kutoka September 24-27 iliyopangwa awali.
Simba Queens, JKT Queens, Yanga Princess na Ceasiaa zitachuana katika michuano hiyo inayoashiria ufunguzi wa msimu mpya wa ligi kuu ya Wanawake
Kwa mara nyingine, itashuhudiwa mechi ya dabi ambapo Simba Queens waliotwaa ubingwa msimu uliopita watachuana na Yanga Princess wakati JkT Queens wakiumana na Ceasiaa Queens katika mechi za Nusu Fainali.
Ratiba ya Nusu Fainali Ngao ya Jamii 2024
👉02 October 2024
13:00 JKT Queens vs Ceasia Queens
16:00 Simba Queens vs Yanga Princess
Ratiba ya Mshindi wa Tatu Ngao ya Jamii 2024
👉05 October-2024
13:00 Looser SF1 vs Looser SF2
Ratiba ya Fainali Ngao ya Jamii 2024
👉05 October-2024
16:00 Winner SF1 vs Winner SF2
Mechi zote hizi zitachezwa kwenye Uwanja wa KMC Complex, Mwenge Jijini Dar Es Salaam.