RATIBA ya Ligi Kuu ya NBC 2024/2025
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB) imetangaza ratiba ya NBC Premier League msimu wa 204/2025 ambayo imeanza kutimua vumbi Agosti 16, 2024 kwa kuishuhudia mechi moja tu kati ya Pamba Jiji dhidi ya Tanzania Prisons na mechi hiyo kuisha Kwa sare tasa.
Je Simba na Yanga zitakutana lini kwa mara ya kwanza Msimu huu wa 2024/2025?, jibu hilo limewekwa wazi na Bodi kama ilivyoanishwa hapa chini?
Kwa mujibu wa ratiba hiyo, watani wa jadi Simba SC na Young Africans watakutana Kwa mara ya kwanza kwenye Ligi October 19, 2024 ambapo Simba SC watakuwa mwenyeji dhidi ya Yanga SC.
Ratiba hiyo pia inaonesha kuwa pazia la NBC Premier League litafungwa mnamo May kwa kushuhudia mechi nane zote zikichezwa muda mmoja saa 10:00 jioni.
Bonyeza hapa chini kupakua ratiba hii.
RATIBA KAMILI YA NBC PREMIER LEAGUE 2024/2024 TAFADHALI BOFYA HAPA