Klabu ya Simba SC imekamilisha usajili wa winga wa kimataifa wa DR Congo, Elie Mpanzu Kibisawala kwa mkataba wa miaka miwili.
Mpanzu mwenye umri wa miaka 22 amesaini mkataba huo kwa dau la dola 200,000 (Milioni 545 za Kitanzania) kama mchezaji huru baada ya mkataba wake na As Vita Club kufikia tamati.
Winga huyo alikuwepo Jana kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa kuwashuhudia wachezaji wenzake wakitinga makundi katika michuano ya kombe la Shirikisho (CAF CC) kwa ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Al Ahli Tripoli ya Libya.
Baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili sasa anaweza kuitumikia Klabu yake ya Simba kuanzia hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Afrika (CAF Confederation Cup 2024/2025).