NAFASI MPYA ZA AJIRA SERIKALINI UTUMISHI (PSRS)
Nafasi mpya za Kazi Kutoka Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma (PSRS) ambayo ni chombo cha serikali chenye hadhi ya Idara inayojitegemea iliyoanzishwa mahususi kuwezesha mchakato wa kuajiri watumishi katika Utumishi wa Umma.
Chombo hiki kilianzishwa kwa Sheria ya Utumishi wa Umma namba 8 0f 2002 iliyorekebishwa na Sheria namba 18 ya mwaka 2007, kifungu cha 29(1).
Dira yake ni Kuwa Kituo cha Ubora katika Utumishi wa Umma katika kanda.
Dhamira yake ni kufanya uajiri wa watumishi wa Umma kwa kutumia mbinu za kisasa kwa kuzingatia misingi ya usawa, uwazi na stahili pamoja na kutoa ushauri kwa waajiri kuhusu masuala ya ajira.
Rasilimali watu ni kigezo muhimu katika utoaji wa huduma za umma, hivyo basi, PSRS imepewa jukumu la kuajiri watumishi wa umma kwa haki, uwazi na kwa wakati; huku tukiangalia na kuhakikisha ubora na upatikanaji kwa waombaji wote ili kutoa huduma yenye usawa nchini Tanzania.
Lengo letu ni kuboresha Utumishi wa Umma wa Serikali kuhusu masuala yanayohusu mchakato wa kuajiri Kulingana na sheria na kanuni zetu na wakati huo huo kuimarisha uhusiano mzuri na wadau wetu.
Chombo hicho kinakaribisha maombi ya Watanzania kujaza nafasi mpya na zilizoachwa wazi mwezi huu October 2024.
BOFYA HAPA KUPATA AJIRA ZOTE ZA SERIKALINI MWEZI HUU OCTOBER 2024BOFYA HAPA KULOGIN AJIRA PORTALBOFYA HAPA KUJISAJILI AJIRA PORTALKUONA AJIRA ZINGINE, WALIOITWA KAZINI NA WALIOITWA KWENYE USAILI TAFADHALI BONYEZA HAPA
Waombaji wa fursa za Ajira mnatakiwa kuhuisha (Update) taarifa zenu kwa kutumia namba ya utambulisho wa Taifa (NIN), kwenye eneo ya Personal Details, aidha mnatakiwa kuhuisha taarifa kwenye eneo la Academic Qualification kwa kuweka kozi yako kwenye Category husika.
Ili kuona ‘STATUS’ ya maombi yako ya kazi, ingia sehemu ya ‘MY APPLICATION’ baada ya ku-‘login’ katika akaunti yako. Sehemu hii itakuwezesha kuona namba ya usaili kwa wale waliofanikiwa na sababu ya kutokuitwa kwa wale ambao hawajafanikiwa.