Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kakonko anayo furaha kutangaza nafasi 10 za ajira ya Vibarua kwa watanzania wote wenye sifa stahiki kwa nafasi ya Vibarua wa usafi nafasi 8 na Waingiza Taarifa katika mfumo wa TASAF MIS nafasi 2.
Nafasi za ajira hizi zinatokana na uhitaji wa Halmashauri wa huduma ya usafi na wasaidizi.
✅Vibarua wa usafi - Nafasi 8
Kazi na Majukumu
- Kufanya usafi wa ndani
- Kufanya usafi wa nje
- Kuandaa kumbi za mikutano
- Kufanya kazi nyingine kadri atakavyoelekezwa na Msimamizi wake.
Sifa za Kuajiriwa.
- Awe anajua kusoma na kuandika
- Muombaji awe na umri kuanzia miaka 18 na usiozidi miaka 45
- Muombaji awe mchapakazi.
- Muombaji awe muadilifu
✅Waingiza Taarifa kwenye mfumo wa TASAF MIS - Nafasi 2
Majukumu ya Kazi
- Jukumu Kubwa ni Kuingiza data kwenye Mfumo TASAF MIS
- Kuingiza taarifa za kaya (Data Update)
- Kusajiri Miradi ya PWP
- Kuingiza taarifa za Mahudhurio ya walengwa waliofanya kazi (mahudhurio ya kazi)
- Kuingiza taarifa za walengwa kwa ajili ya kutimiza masharti ya Elimu na Afya Kusajili vikundi vya COMSIP
- Kuingiza taarifa za fedha kwa wanavikundi vya kuweka akiba na kuwekeza na Uncollected
- Kuingiza mipango kazi ya Biashara na Taarifa za malipo za walengwa Pamoja na majukumu mengine utakayopangiwa na mkuu wako wa kazi
SIFA ZA MWOMBAJI
- Wahitimu wa kidato cha nne
- Awe ana ujuzi wa kutumia Komputya Muombaji awe mchapakazi
- Muombaji awe muadilifu
Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 12/09/2024 saa tisa na nusu alasiri. Maombi yote yatumwe kwa kutumia anuani ifuatayo;-
Mkurugenzi Mtendaji,
Halmashauri ya Wilaya,
S.L.P. 03,
KAKONKO.
Tags
Ajira