Klabu ya Simba imefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa kirafiki kati ya uliopigwa uwanja wa KMC Complex leo Jumamosi 07 September 2024.
Mabao ya Jean Charles Ahoua na Saleh Karabaka yametosha kuihakikishia Simba ushindi huo ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea mchezo wa kuwania kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho (CAF CC) dhidi ya Al Ahly Tripoli.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa kati ya September 14 na 15.