Bao pekee la beki wa kati, Ibrahim Abdallah dakika ya 13 limewahakikishia ushindi Young Africans wa bao 1-0 dhidi ya Ken Gold ya Mbeya katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
Ushindi huo unakuwa wa pili kwa Young Africans katika mechi zake mbili za mwanzo wa msimu 2024/2025, baada ya ushindi wa awali wa mabao 2-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Ken Gold FC ya Chunya Mbeya ikiwa imepanda Ligi Kuu msimu huu Sasa inafikisha mechi tano bila ushindi wala sare, wakifungwa Mechi zote.