Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba anapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi ya Mtendaji wa Mtaa Daraja la III waliofanya usahili tarehe 24/09/2023 na tarehe 25/09/2023 kuwa wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Database) kwa kada hiyo wanaitwa kazini baada ya nafasi kupatikana.
Waombaji kazi wanaoitwa wanatakiwa kuripoti Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba ndani ya siku saba (7) kutoka tarehe ya tangazo hili wakiwa na vyeti halisi (Original Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na Mwajiri kabla ya kupewa barua ya Ajira.
Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/ hawakufaulu usahili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa.
MUHIMU: Wakati wa kuripoti wahusika wanapaswa kuwa na kitambulisho kwaajili ya utambuzi, na vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na; Kitambulisho cha Uraia, Hati ya kusafiria, Kitambulisho cha Mzanzibari Mkaazi, Kitambulisho cha Mpiga Kura au Leseni ya Udereva.
KUONA MAJINA YA WALIOITWA KAZINI DONWLOAD PDF HAPA