Waombaji wote wa vyeti vya kuzaliwa wanatakiwa kufuata muongozo ufuatao;
- Ingia kwenye tovuti ya erita.rita.go.tz/auth
- Bonyeza REGISTER katika kipengele cha REGISTRATION na jaza taarifa zote kwa usahihi kufungua akaunti ya maombi;
- (Muhimu: Nenosiri (Password) liwe na herufi zaidi ya nane ikiwa na herufi kubwa, ndogo, namba na alama yoyote mfano (@\#*&) 05.
- Ingia katika akaunti ya barua pepe "email" fungua ujumbe uliotumiwa kutoka RITA kisha bonyeza neno "Account activation"
- Baada ya kufungua akaunti, Bonyeza SIGN IN na jaza taarifa sahihi ili kuingia katika mfumo;
- Chagua BIRTH SERVICES kwa huduma ya Kizazi (DEATH SERVICES) kwa huduma ya kifo);
- Chagua REQUEST VERIFICATION na jaza taarifa zote kwa usahihi;
- Chagua VERIFICATION REASON ambapo uchague TAASISI inayohitaji uhakiki mfano: LOANS BOARD, NHIF N.K
- Ambatanisha Cheti cha Kuzaliwa/kifo kinachohakikiwa;
- Omba namba ya Malipo kwa kubonyeza "REQUEST CONTROL NUMBER"
- Fanya malipo sahihi kulingana na Ankara uliyopewa;
Kumbuka: Majibu ya Uhakiki yatatumwa kupitia akaunti uliyofungua.
Muhimu:
- Tunza nywila/ nenosiri la akaunti uliyofungua
- Ambatanisha Kivuli (copy) katika mfumo wa PDF ambacho taarifa zote ikiwa pamoja na namba ya ingizo (entry number) zinasomeka vizuri.