ADA YA MAOMBI YA PASIPOTI na HATI YA KUSAFIRI

ADA YA MAOMBI YA PASIPOTI na HATI YA KUSAFIRI

ADA YA MAOMBI YA PASIPOTI na HATI YA KUSAFIRI

HATUA ZA UJAZAJI FOMU YA MAOMBI YA PASIPOTI KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI (MTANDAO).

  1. INGIA KATIKA TOVUTI YA IDARA: www.immigration.go.tz KISHA NENDA KATIKA KITUFE CHA e-SERVICES
  2. CHAGUA PASSPORT APPLICATION FORM;
  3. CHAGUA OMBI JIPYA;
  4. TIKI KIBOKSI KUKUBALIANA NA MAELEKEZO;
  5. JAZA TAARIFA ZAKO KWA UKAMILIFU UKIFUATA MAELEKEZO NA MPANGILIO (FORMAT) KATIKA KILA KIPENGELE;

NB: BAADA YA MWOMBAJI KUKAMILISHA KUJAZA TAARIFA ZAKE, ATAFAHAMISHWA YA KWAMBA USAJILI UMEKAMILIKA NA KUPATIWA NAMBA YA OMBI, AMBAYO NI MUHIMU AIANDIKE PEMBENI NA KUIHIFADHI KWA KUMBUKUMBU ZA BAADAE.

KISHA ATAPEWA NAMBA YA KUMBUKUMBU YA MALIPO (CONTROL NUMBER) NA KUTAKIWA KWENDA KULIPIA MALIPO YA AWALI (ADVANCE FEE) YA TSH 20,000.

BAADA YA KUKAMILISHA USAJILI, NA KUPATIWA NAMBA YA OMBI NA NAMBA YA KUMBUKUMBU (CONTROL NUMBER), UKURASA UTAONEKANA KAMA IFUATAVYO:

UTARATIBU WA MALIPO YA ADA YA HUDUMA YA PASIPOTI KWA KUTUMIA M-PESA/TIGOPESA

INGIA KWENYE MENU YA M-PESA/TIGOPESA (*150*00#/*150*01#)

  1. Bonyeza Namba 4 (Lipa kwa M-Pesa) - VODA
  2. Bonyeza Namba 4 (Kulipia Bili) - TIGO

Kisha Weka/Ingiza Namba ya Kampuni

  1. Ingiza Namba (888999)
  2. Ingiza kumbukumbu Namba(Ingiza Control Number inayoanzia na 99109…….)
  3. Ingiza kiasi (kama ulivyo elekezwa Mfano: 20,000 nk.)
  4. Utapata Maelezo kuwa unalipa pesa NMB
  5. Ingiza Namba ya Siri
  6. Hakiki
  7. Utapata Meseji toka M-Pesa/Tigopesa kama muamala umekubalika;

Utapata meseji kutoka kwenye mfumo Namba 15200
kama muamala umekubalika;

  1. Mteja atatakiwa kurudi katika OMBI LINALOENDELEA:
  2. Kisha ataingiza NAMBA YA OMBI/SIMU na NAMBA YA RISITI

Na hapo ataweza kupakua Fomu yake ya Maombi

Ataiwasilisha Fomu hiyo katika Ofisi ya Uhamiaji Makao makuu au Afisi Kuu Zanzibar

UTARATIBU WA MALIPO YA ADA YA HUDUMA YA PASIPOTI KWA KUTUMIA BENKI NMB/CRDB

  1. Jaza fomu ya malipo ya kielectroniki;
  2. Fuata maelekezo kama yanavyojieleza kwenye fomu;
  3. Utapata meseji toka benki;

           Utapata meseji toka kwenye mfumo Namba 15200  

     kama muamala umekubalika.

Fomu ya maombi20,000/=15
AINA

ADA

TANZANIA

ADA

UBALOZI (USD)

PASPORT YA KAWAIDA YA KIELEKTRONIKI130,000/=                         75
HUDUMA PASIPOTI YA KIELEKTRONIKI130,000/=                          75
PASIPOTI YA KIELEKTRONIKI YA KIDIPLOMASIA130,000/=                          75
HATI YA USAFIRI WA DHARURA20, 000/=                          20
CHETI CHA KITAMBULISHO10,000/= 
HATI YA KUSAFIRI YA MKUTANO MKUU20,000/= 

NB: Dola 90 za Marekani kwa waombaji wa pasi za kusafiria wanaotuma maombi kutoka nje ya Tanzania hulipwa kikamilifu kama ada ya pasipoti mbali na gharama nyinginezo ambazo zinaweza kutozwa na benki kama ada ya muamala.

Passport online Application Tanzania, Bei ya passport Tanzania 2023, Maombi ya passport mpya Tanzania, Fomu ya maombi ya passport, Maombi ya Passport online, Gharama za kupata Passport Tanzania, Inachukua muda gani kupata passport mpya.

Njia ya Malipo ya Pasipoti kupitia Mabalozi.

Waombaji wa Pasipoti kupitia Mabalozi wanatakiwa kujaza fomu ya maombi Mtandaoni, na kulipa USD 90 yote ambayo inagharamia ada ya Maombi (USD 15) na ada ya Pasipoti (75 USD).

Kwa hiyo, baada ya kujaza fomu mtandaoni, mwombaji atapewa nambari ya udhibiti ya 90USD (kwa maombi ya kawaida) na  USD 265 kwa wale waliopoteza pasipoti zao na kutuma maombi kama mwombaji aliyepotea.

Kwa hiyo, waombaji wanashauriwa sana kuhakikisha kuwa wana hati za kutosha na kuomba aina sahihi ya pasipoti kabla ya kufanya malipo.

Njia ya Malipo kwa Waombaji wa Pasipoti wakiwa Tanzania.

Waombaji wa pasi za kusafiria wanaojaza na kutuma maombi yao kutoka ndani ya nchi wanatakiwa kufanya malipo yao katika sehemu mbili (20,000 kama ada ya fomu ya maombi) na (130,000 kama ada ya pasipoti).

Aidha Ada ya pasipoti inalipwa wakati mwombaji anawasilisha maombi yake.

Post a Comment (0)
Previous Post Next Post

PATA NYIMBO ZOTE MPYA BONYEZA HAPA

 

MATANGAZO YA BIASHARA WASILIANA NASI KUPITIA nijuzehabariblog@gmail.com

 

JIUNGE NA GROUP ZETU HAPA CHINI UPATE FURSA KAMA HIZI KILA SIKU.

 

GROUP LA WHATSAPP NO 1 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 2 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 3 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 4 BOFYA HAPA

 

GROUP LA WHATSAPP NO 5 BOFYA HAPA